OFISI YA AFISA MDHAMINI - ORTMSMIM (OFISI KUU PEMBA)

Ofisi ya Afisa Mdhamini ni kiungo kati ya Taasisi za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ zilizopo Pemba ikiwa na jukumu kuu la kuratibu na kusimamia kazi zote za Ofisi kwa upande wa Pemba.

 

 UONGOZI

Kiongozi mkuu (Afisa Mdhamini) wa shughuli za ORTMSMIM kwa upande wa Pemba niNd. THABIT OTHMAN ABDALLA 

MAJUKUMU YA OFISI YA AFISA MDHAMINI (KWA UPANDE WA PEMBA)

  • Kuratibu shughuli zote zinazofanywa na ORTMSMIM.
  • Kuratibu na kuwasilisha ripoti au taarifa za utekelezaji za kila robo, nusu na mwaka kwa Katibu Mkuu wa ORTMSMIM.
  • Kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.
  • Kuratibu taarifa za bajeti na hotuba ya makadario ya mapato na matumizi.
  • Kuratibu,kushauri,kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za Serikali za mitaa na Mamlaka zake.
  • Kufuatilia na kukagua utendaji wa Serikali za Mitaa katika kutoa huduma.
  • Kuimarisha utawala bora na kuimarisha uwezo wa Serikali za Mitaa katika utoaji wa huduma.

Wasiliana nasi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

2277 Barabara ya Vuga,

S.L.P 4220,

70401 Mjini Magharibi,

Tel: +255242230034

Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Waliotembelea Tovuti

3752332
Today
Yesterday
This Week
This Month
All days
297
477
2216
7912
3752332