IDARA YA UTUMISHI NA UENDESHAJI:

MUUNDO
ORG3

1. MKURUGENZI
Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi ni Ndugu JUMA NYASA JUMA.

MAJUKUMU

  • Kutoa huduma za uongozi wa Rasilimali Watu na Utawala kwa wizara husika. 
  • Kusimamia makujumu ya vitengo vilivyo chini ya Idara.
  • Kusimamia masuala ya ajira, mafunzo, kupandishwa vyeo kwa wafanyakazi wa Wizara.
  • Kuhakikisha kuwepo kwa watendaji wa kutosha na wenye sifa na kuweka kumbukumbu za masuala mbalimbali yahusuyo watendaji.
  • Kufanya tathmini ya utendaji wa kila mtumishi wa Wizara na kuandaa ripoti ya hali ya utumishi kila baada ya muda kwa mujibu wa matakwa ya sheria au maagizo maalum.
  • Kuratibu masuala mtambuka yakiwemo (Ukimwi, Jinsia, Mabadiliko ya  hali ya nchi, mambo ya idadi ya watu).
  • Kutoa huduma za kitaalamu na huduma za manunuzi na uhifadhi wa vifaa kwa ajili ya Idara nyengine.
  • Kutoa huduma za uhasibu ikiwa ni pamoja na uwekaji wa kumbukumbu za hesabu, mapato na matumizi, ulipaji wa mishahara na matayarisho ya mafao ya uzeeni.
  • Kuandaa na kusimamia mpango kazi wa Idara.
  • Kuandaa na kusimamia bajeti ya Idara.
  • Kufanya kazi nyenginezo kama zitakavyoelekezwa na Uongozi wa Wizara kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za kazi.

2. KITENGO CHA UENDESHAJI
Kinaongozwa na Ofisa Utawala Mkuu.

MAJUKUMU

  • Kuweka kumbukumbu za matukio muhimu katika sehemu ya kazi. 
  • Kusaidia kusimamia nidhamu  ya wafanyakazi.
  • Kuainisha matatizo ya wafanyakazi.
  • Kusimamia matumizi na matunzo ya vifaa vya wizara ikiwemo vyombo vya usafiri, magari, mitambo, samani, vifaa vya kuandikia na vifaa vya mawasiliano.
  • Kusimamia majengo na mali nyengine zisizohamishika.
  • Kusimamia shughuli za kiufundi na uendeshaji wa maghala ya Wizara.
  • Kufanya kazi zote atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi. 

3. KITENGO CHA UTUMISHI
Kinaongozwa na Ofisa Mkuu Utumishi.

MAJUKUMU

  • Kutunza kumbukumbu sahihi za watumishi wote kulingana na mahali alipo. 
  • Kukusanya takwimu na kumbukumbu zote zinazohusu mipango ya watumishi.
  • Kusaidia kukadiria idadi ya watumishi wanaohitaji mafunzo.
  • Kufanya kazi zote atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi.

4. KITENGO CHA UTUNZAJI KUMBUKUMBU
Kinaongozwa na Ofisa Kumbukumbu Mkuu.

MAJUKUMU

  • Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji. 
  • Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka.
  • Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi kulingana na somo husika (classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya ofisi.
  • Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki (file racks/cabinets) katika masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu.
  • Kuweka kumbukumbu (barua, nyaraka nk.) katika mafaili.
  • Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali.
  • Kufanya kazi nyengine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi. 

Wasiliana nasi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

2277 Barabara ya Vuga,

S.L.P 4220,

70401 Mjini Magharibi,

Tel: +255242230034

Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Waliotembelea Tovuti

3716305
Today
Yesterday
This Week
This Month
All days
266
71
2504
19662
3716305