• HAFLA YA KUWAAGA WASTAAFUNaibu katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mikidadi Mbarouk Mzee amewataka wastaafu wa ofisi hiyo kuendeleza mazuri waliyoyapata katika kipindi chote cha utumishi wao..
  • UFUNGUZI WA SOKO LA MWANAKWEREKWERais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akishirikiana na Waziri wa Nchi OR-TMSEMIM Mh Masoud Ali Mohammed katika ufunguzi wa Soko la Mwanakwerekwe.
  • UTIAJI WA SAINI WA JAA LA KIBELEKatibu Mkuu Ofisi ya Raisi Tawala Za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Ndugu Issa Mahfoudh Haji na Mr Ariff kutoka kampuni ya Envigenic wakitiliana saini ya amkubaliano ya kusafisha jaa kubwa la Kibele.
  • WAFANYAKAZI WA OR-TMISEMIMWafanyakazi wa Ofisi Y Rais Tawla Za MIkoa Serikali Za Mitaa Na Idara Maalum Za SMZ Wakiwaaga Watumishi waliomaliza muda wao katika Wizara hiyo.
  • UWASILISHAJI WA BAJETI BARAZA LA WAWAKILISHIWaziri wa Nchi Ofisi Ya Raisi Tawala Za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Akiwasilisha Bajeti ya Wizara katika Baraza la Wawakilishi.
  • ZIARA ZA  MASOKORais wa Zanzibar dk Huseein Ali Mwinyi akishirikiana na Waziri Masoud Ali Mohd Katika kufanya Ziara za Kutembelea Masoko yanayoendelea na Ujenzi.
  • TAMASHA LA MAONYESHO YA BIASHARAWafanyakazi wa OR-TMISEMIM wakishiki katika Tamasha la Maonyesho ya Biashara ya Mapinduzi kuadhimisha Miaka 61.
  • MIAKA MINNE YA DR HUSSEIN ALI MWINYIWaziri wa OR-TMSEMIM Mh Msoud Ali Mohammed akiwasilisha Ripori ya Mafanikio ya Rais wa Zanzibar katika kutimiza miaka minne ya Uongozi wake.
OR-TAMISEMIM-HABARI

Angali Habari Zote

UZINDUZI WA MICHEZO YA KIJESHI

Rais wa Zanzibar Dr Hussein Ali Mwinyi Azindua Mafunzo ya KIjeshi


Read More

WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAISI TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ

MHE MASOUD ALI MOHAMMED

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ, Mh, Masoud Ali Mohammed,amesema ujenzi wa ofisi za masheha katika shehia itawawezesha kuongezeka uwajibikaji na wananchi kuwa huru pindi wanapofata huduma. Akitembelea ujenzi wa Ofisi ya Sheha shehia ya Ijitimai Mwanakwerekwe, amemtaka mkandarasi wa ujenzi huo Kikosi cha KVZ Kuharakisha ujenzi huo ili kuwawezesha masheha kuongeza ufanisi wa kiutendaji kwa wakaazi wao. Mkuu wa Wilaya ya Magharib 'B', Hamida Mussa Khamis, amesema anamatarajio kwa Masheha kuleta mabadiliko na kuwaondoshea mazingira magumu ya kazi waliyokumbana nayo hapo kabla. Mkandarasi wa ujenzi huo Mkuu wa Kikosi cha Valantia KVZ, Luten kanal Said Ali Shamhuna, amesema ujenzi huo umezingatia kiwango cha ubora kinachosimamiwa na Wakala wa Majengo ZBA na kuahidi kukamilika kwa wakati uliopangwa. Nae Sheha wa shehia ya Ijitimai Rashid Mwadini Omar, pamoja na mwananchi wa shehia hiyo wamepongeza hatua ya Serikali kuwajengea Ofisi ambazo zitaleta ufanisi na usiri wa kazi, tofauti na hapo awali. Jumla ya Ofisi 388 zinatarajiwa kujengwa kwa kila wilaya za Unguja na Pemba . Imetolewa na kitengo cha Habari na Uhusiano Or-tamisemim Zanzibar