KAMATI YA KUSIMAMIA OFISI ZA VIONGOZI WAKUU WA KITAIFA YA BARAZA LA WAWAKILISHI
Mwenyekiti wa kamati ya kusimamia viongozi wakuu wa kitaifa ya Baraza la Wawakilishi, Mh Machano Othman Said, akizungumza baada ya kutembelea Vikosi vya Idara Maalum, amesema wamebaini kuwa vikosi hivyo vinaendesha miradi yake ya uzalishaji bila ya kuwa na utaalamu wa kutosha na kupelekea kushindwa kujitegemea.
ZIARA YA UJUMBE WA INDIA NAVY UKIONGOZWA NA KOMODOO AGYAPAL SINGH
Akizungumza na ujumbe wa India Navy Ofisini kwake Vuga, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mh. Masoud Ali Mohammed, Amesema ushirikiano huo utahusisha uthibitisho wa Biashara haramu ya usafirishaji binaadamu na Dawa za kulevya na kupambana na uharamia.
UZINDUZI WA MAGARI YA USAFI KWA MANISPAA MAGHARIBI A
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ, Mh Masoud Ali Mohammed, amesema kukabidhiwa magari ya taka iwe ni kuleta mageuzi ambayo yatachangia kuweka miji katika mazingira mazuri.
MAKABIDHIANO YA VIFAA VYA USAFI
Mh.Masoud Ali Mohammed, akikabidhi vifaa hivyo kwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa mjini, amesema Jamhuri ya watu wa China imekuwa na uhusiano mzuri na Zanzibar na kuunga mkono jitihada za kimaendeleo ikiwemo za kuimarisha usafi wa miji.
MATEMBEZI YA MH. RAIS HUSSEIN MWINYI AKIZUNGUMZA NA MAAFISA KIKOSI CHA KUZUIA MAGENDO ZANZIBAR (KMKM) KIBWENI NA KIKOSI CHA KVZ MTONI MKOA WA MJINI MAGHARIBI IKIWA NI MWENDELEZO WA ZIARA YAKE YA KUTEMBELEA VIKOSI VYA SMZ
Kamanda Mkuu wa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza Maafisa, Askari na Wapiganaji wa Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kudumisha nidhamu, uzalendo , uwajibikaji na uadilifu.
ZIARA YA MH.HUSSEIN ALI MWINYI AKITEMBELEA VIKOSI VYA ZIMAMOTO NA UOKOZI, JKU NA CHUO CHA MAFUNZO IKIWA NI MWENDELEZO WA ZIARA YAKE YA KUTEMBELEA VIKOSI VYA SMZ
Kamanda Mkuu wa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amevipongeza Vikosi vya Jeshi la Kujenga Uchumi(JKU), Zimamoto na Uokozi na Chuo cha Mafunzo kwa ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa madarasa, masoko na vituo vya wajasiriamali.
UKAGUZI WA UJENZI WA MADUKA UNAOENDELEA AWAMU YA PILI DARAJANI SOUK
Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Mh: Masoud Ali Mohammed, amewataka wakandarasi wa ujenzi wa maduka Darajani, kulifanya eneo hilo kuwa kivutio kwa watumiaji.
KIKAO CHA WATENDAJI WA MABARAZA YA MANISPAA, MABARAZA YA MJI NA HALMASHAURI
Akizungumza na Wakurugenzi, Mameya na Wenyeviti wa kamati za Madiwani, makao makuu ya Kikosi cha Valantia Mtoni, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mh Masoud Ali Mohammed, amesema mivutano baina yao imekuwa ikizorotesha upatikanaji huduma muhimu kwa wananchi.
HAFLA YA KUWAAGA WAFANYAKAZI WASTAAFU WATATU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ mh Masoud Ali Mohammed amewataka watendaji kuzingatia kanuni na sheria za utumushi wa umma ili kuleta ufanisi katika kazi zao.
KUKABIDHIANA BENDERA NA MIHURI YA KISASA KATIKA MAKAO MAKUU YA KVZ MTONI
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa Serikali za mitaa na Idara Maalum za SMZ mh Masoud Ali Mohammed, amesema Masheha wakitekeleza majukumu yao kwa uadilifu bila hofu hakuna adui atakaejaribu kuchezea amani iliyopo nchini.
ZIARA YA SEHEMU INAYOTARAJIA KUJENGWA MRADI WA MAEGESHO NA SEHEMU YA KUPUMZIKIA KATIKA BWAWA LA MWANAKWEREKWE SOKONI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Mh Masoud Ali Mohammed, amesema mradi wa maegesho katika bwawa la mwanakwerekwe ufanyiwe utafiti wa kina ili kuepusha uharibifu wa miundombinu.
SHEREHE YA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA MAPINDUZI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi ameongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
MKESHA WA FASHIFASH
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amejumuika pamoja na Viongozi mbalimbali na wananchi katika Tamasha la Burudani na Urushaji wa Fashifash viwanja vya Maisara Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 11 Januari 2024.
UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SOKO KUU LA MWANAKWEREKWE WILAYA YA MAGHARIBI B
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar mpya itakuwa na usafiri wa umma wa mabasi ya umeme, treni pamoja na Taxi za baharini.
UZINDUZI WA SOKO LA MAMA LISHE KINYASINI MKOA WA KASKAZINI UNGUJA
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Mchezo Mhe. Tabia Maulid Mwita amesema ujenzi wa Miradi ya Maendeleo ni nija bora ya kuyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar Kivitendo.
UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI KATIKA OFISI YA MAKAO MAKUU YA CHUO CHA MAFUNZO
Makamu wa pili wa rais wa zanzibar mstaafu balozi seif ali idd amesema serikali ya mapinduzi ya zanzibar ina wajibu wa kuhakikisha maafisa na askari wanafanya kazi katika mazingira mazuri ikiwa ni haki yao ya msingi.
UZINDUZI WA OFISI YA ZIMAMOTO NA UOKOZI KANDA YA KASKAZINI UNGUJA
Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Mh Rahma Kassim Ali, amesema ujenzi kwa Afisi ya Zimamoto kanda ya Kaskazini ni jitihada za Serikali za kuhakikisha maisha ya wananchi yanakuwa salama pamoja na wawekezaji wanaowekeza katika sekta ya utalii katika ukanda huo.
UFUNGUZI WA SOKO LA MATUNDA NA MBOGA MBOGA DONGE MTAMBILE
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na utawala bora, Mh Haroun Ali Suleiman, amesema serikali itaendelea kuvitumia vikosi vya Idara Maalum za SMZ katika ujenzi wa miradi ya maendeleo.
UWEKAJI WA JIWE LA MSINGI SOKO LA JUMBI
Rais mstaafu wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein, amesema Mapinduzi ya Zanzibar, yamefanyika kwa ajili ya wananchi kupata uhuru na kufikia hatua za maendeleo.
UWEKAJI JIWE LA MSINGI SOKO LA CHUINI
Makamu wa Pili wa Rais Mh Hemed Suleiman Abdulla, amesema serikali itahakikisha inaimarisha maslahi ya wananchi, kwa kuwawekea mazingira mazuri.
UWEKAJI JIWE LA MSINGI SOKO LA CHUINI
Makamu wa Pili wa Rais Mh Hemed Suleiman Abdulla, amesema serikali itahakikisha inaimarisha maslahi ya wananchi, kwa kuwawekea mazingira mazuri.
Ujumbe wa Waziri

waziripaspotiMnamo Tarehe 19, Novemba 2020 Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi alitangaza Muundo wa Wizara pamoja na Baraza la Mawaziri, ambapo alimteuwa Mheshimiwa Massoud Ali Mohammed (Mwakilishi wa wananchi Jimbo la Ole) kuwa Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ (OR-TMSMIM).

Muundo wa Afisi hii unajumuisha Afisi za Wakuu wa Mikoa, Afisi za Wakuu wa Wilaya, Jiji,  Manispaa, Mabaraza ya Miji na Halmashauri.

Kadhalika Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii, Afisi ya Asasi na Jumuiya zisizokuwa za Serikali (NGO's), Viwanda vya Idara Maalum za SMZ, pamoja na Idara Maalum za SMZ ambazo ni:-

1. Kikosi Maalum Cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM).

2. Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKUZ).

3. Idara ya Chuo cha Mafunzo (MF).

4. Idara ya Zimamoto na Uokozi (KZU).

5. Idara ya Valantia (KVZ).

Aidha kwa mujibu wa ibara ya 123(1) Kamanda Mkuu wa Idara Maalum za SMZ ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Ambapo Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ndie msimamizi wa Afisi inayosimamia Idara Maalum za SMZ.

Katika kutekeleza malengo ya uanzishwaji wa Wizara hii Afisi itahakikisha misingi ya uwajibikaji, uwazi, ufanisi na kujitolea katika ngazi zote za uongozi wa Wizara.

HISTORIA

Kabla ya Mapinduzi ya januari 1964, wananchi walikua hawashirikishwi katika katika maamuzi kuhusu ustawi wa maendeleo yao. Mtiririko wa ngazi za utawala ulikua ni wa kupokea amri na kusimamia utelezaji wa amri hizo ambazo huanzia ngazi ya juu ya...

Soma Zaidi

Dira

Kuwa taasisi imara katika kusimamia amani, usalama, usajili wa wakaazi na upatikanaji wa huduma karibu na wananchi.

 

 

Dhamira

Kujenga mazingira mazuri ya ushiriki wa wananchi katika kudumisha amani ulinzi wa mali zao, kuimarisha huduma za kijamii, kuhakikisha kuwa jamii inashiriki katika kupanga na kusimamia shughuli za maendeleo katika maeneo yao kwa kuzingatia misingi ya utawala bora ikihusisha kuwatambua wakaazi wa maeneo husika na utambulisho wao.

 

Majukumu

Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ ina majukumu makuu yafuatayo:-

  1. Kusimamia Sera, Sheria na Kanuni mbali mbali za Ofisi.
  2. Kubuni na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Soma zaidi

Wasiliana nasi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

2277 Barabara ya Vuga,

S.L.P 4220,

70401 Mjini Magharibi,

Tel: +255242230034

Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Waliotembelea Tovuti

3694042
Today
Yesterday
This Week
This Month
All days
597
823
4111
21484
3694042